Wafuasi na wakosoaji wa serikali ya Eritrea wanashiriki katika mapigano makali katika hafla ya kuunga mkono serikali huko Tel Aviv.
Zaidi ya watu 100 wamejeruhiwa katika mapigano kati ya makundi hasimu ya waandamanaji kutoka Eritrea katika mji wa Tel Aviv nchini Israel huku polisi wakifyatua risasi za onyo angani kuwatawanya waandamanaji hao.
Mapigano yalizuka siku ya Jumamosi baada ya mamia ya raia wa Eritrea waliokosoa serikali yao kufika mahali ambapo hafla inayoiunga mkono serikali ilikuwa ikifanyika.

Post a Comment