Mwinjilisti maarufu wa televisheni nchini Kenya Mchungaji Ezekiel Odero ameshutumu wanaume wanaowapa ujauzito wanawake kisha kuwatupa pamoja na watoto.
Katika mahubiri yake ya hivi majuzi, Mchungaji Ezekiel alitafakari changamoto wanazokabiliana nazo wale walioachwa kulea watoto peke yao, akimrejelea “msanii maarufu wa bongo fleva” ambaye ameingia kwenye vichwa vya habari kuhusu mahusiano yake.
"Kuna msanii maarufu wa bongo ambaye ana mazoea ya kuwapa ujauzito wanawake tofauti. Amezaa watoto kadhaa na wanawake mbalimbali. Na wakati anawapenda, wasichana hawa hawajali. Wanadhani ni wao tu atachumbiana nao,” Mchungaji Ezekiel alihubiri.
Mchungaji huyo alieleza kuwa safari ya maisha ya msanii huyo imemkuta akiwa na watoto na wanawake tofauti na kisha kuachana.
“Alichukua mmoja kutoka Kenya na kumpa ujauzito kisha kumtupa. Hana roho ya ndoa."
CHANZO KENYA GHAFLA

Post a Comment