Jopo la uchunguzi wa kihistoria kuhusu madai ya ukiukaji wa haki za binadamu uliyofanywa na wanajeshi wa Uingereza nchini Kenya limekuwa likipokea ushahidi "wa kuhuzunisha" kutoka kwa wale wanaosema walidhulumiwa.
Makumi ya watu wiki hii wametoa ushahidi mbele ya kamati ya bunge kuhusu madai ya utovu wa nidhamu wa wanajeshi kutoka Kitengo cha Mafunzo ya Jeshi la Uingereza Kenya (Batuk).
Miongoni mwao ni familia ya msichana anayedaiwa kulemaa baada ya kugongwa na na lori la Jeshi la Uingereza, mama ambaye anasema alitelekezwa akiwa mjamzito na mwanamume aliyevamiwa na simba kufuatia moto unaodaiwa kuwashwa wakati wa zoezi la mafunzo ya kijeshi.

Post a Comment