#-----------Start surfernetwork.com--------------- # Ads.txt last updated on:  2026/06/10 13:26:00.23423 by surfernetwork.com MANAGERDOMAIN=surfernetwork.com CONTACT=support@surfernetwork.com # SurferNETWORK surfernetwork.com, 204, DIRECT # Adswizz adswizz.com, 724, RESELLER, 52ded3ee71b94c84 #Azerion targetspot.com, 455, RESELLER, feb28ed826dcf532 improvedigital.com, 2734, RESELLER adswizz.com, 172, RESELLER, 52ded3ee71b94c84 appnexus.com, 7265, RESELLER, f5ab79cb980f11d1 tritondigital.com, 44733, RESELLER, 19b4454d0b87b58b rubiconproject.com, 9753, RESELLER, 0bfd66d529a55807 #US rubiconproject.com, 16418, RESELLER, 0bfd66d529a55807 #EMEA # DAX thisisdax.com, 5460, RESELLER thisisdax.com, 5461, RESELLER # katz Katzdigital.com, 318, RESELLER Katzdigital.com, 80, RESELLER # Magnite rubiconproject.com, 8441, RESELLER, 0bfd66d529a55807 #-----------End surfernetwork.com-----------------

Kamati za Kudumu za Bunge zaanza kukutana Jijini Dodoma



Shughuli za Kamati za Kudumu za Bunge zimeanza kufanyika Jijini Dodoma tarehe 1 Agosti, 2024 na zinatarajiwa kuendelea hadi tarehe 25 Agosti, 2024 kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Kumi na Sita wa Bunge ambao unatarajiwa kuanza kufanyika siku ya Jumanne tarehe 27 Agosti, 2024.


Shughuli zitakazotekelezwa wakati wa Vikao vya Kamati za Bunge katika kipindi hicho ni kama ifuatavyo:-


a. Kuchambua Miswada ya Sheria

Shughuli hii itatekelezwa na Kamati nne (4) za Bunge ambazo ni Kamati ya Utawala, Katiba na Sheria, Kamati ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Kamati ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo na Kamati ya Miundombinu.


b. Kuchambua Sheria Ndogo

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo, itafanya Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa Bungeni katika Mkutano wa Kumi na Tano pamoja na kuchambua taarifa za Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge yatokanayo na Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa Bungeni katika Mkutano wa Kumi na Mbili na Kumi na Tatu.


c. Kupokea Taarifa za Utendaji wa Serikali na Taasisi zake

Kamati kumi na moja (11) za kisekta zitapokea na kujadili taarifa mbalimbali za utendaji wa Serikali na Taasisi zake.Aidha, Kamati ya Bajeti itapokea taarifa mbalimbali kutoka Serikalini kwa lengo la kufuatilia utekelezaji wa shughuli za Wizara ya Fedha na masuala yanayohusu vyanzo vya mapato ya Serikali.


d. Kuchambua Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali

Kamati mbili (2) zinazosimamia matumizi ya fedha za umma, zitachambua Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuhusu Hesabu za Wizara, Mashirika ya Umma na Mamlaka za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2023.


e. Kuchambua Taarifa za Uwekezaji wa Mitaji ya Umma

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) itapokea na kuchambua taarifa za uwekezaji wa mitaji ya umma ili kubaini iwapo uwekezaji huo una ufanisi na kwamba umezingatia taratibu na miongozo mujarabu ya biashara.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Mobile Logo Settings

Usa River Tv