Bonnah Segerea Cup inatoa fursa kwa timu mbalimbali za soka kutoka Segerea na maeneo jirani kushiriki, na inaimarisha umoja na mshikamano kati ya wakazi wa eneo hilo. Pia, mashindano haya yanahamasisha vijana kujihusisha na michezo kama njia ya kujenga afya bora na kuondoa vijana katika maovu.
Mbunge wa Segerea anachangia katika kufanikisha mashindano haya kwa kusaidia rasilimali na vifaa mbalimbali, huku akihamasisha wadhamini na wanajamii kushiriki. Mashindano haya yamekuwa na mafanikio makubwa na yanatarajiwa kuendelea kukua mwaka hadi mwaka.
Kupitia kurasa wake wa kijamii wa facebook Mh Bonnah ameandika "Sisi kwetu michezo ni Ajira, Michezo ni Afya, Michezo kwetu ni burudani, Michezo kwetu ni sehemu ya kujifunza mambo mbalimbali Juu ya Maisha, Michezo Kwetu ni Sehemu ya Kupenyeza Agenda za Maendeleo! Kwa kifupi Michezo ni Sehemu ya Jimbo La Segerea na hatubagui Jinsia.
JIMBO LA SEGEREA x BONNAH SEGEREA CUP. 🔥
#BonnahKazini #JimboLaSegerea #WanawakeNaMichezo
Post a Comment