Liverpool imekuwa na mfululizo wa usajili wenye mafanikio katika miaka ya hivi karibuni, na wachezaji wengi wapya wamefanikiwa kuchangia mara moja. Sasa, klabu hiyo inatarajia kuendelea na mwenendo huo katika majira ya joto ya 2025.
Klabu hiyo kutoka Anfield imekuwa ikitafuta wachezaji wakili wa hadhi ya juu kwa miezi kadhaa, na lengo ni kujenga kikosi kinachoweza kushindana katika mashindano mbalimbali wakati wa msimu wa 2025-26.
Usajili na Kuuzwa wa Liverpool Majira ya Joto 2025
Jeremie Frimpong (Bayer Leverkusen) – Liverpool tayari imemaliza usajili wa nyota wa Bayer Leverkusen kama mbadala wa Trent Alexander-Arnold, ambaye amehamia Real Madrid. Frimpong anatarajiwa kuimarisha upande wa kulia wa ulinzi na mashambulizi.
Florian Wirtz (Bayer Leverkusen) – Klabu iko katika hatua za mwisho za kumaliza usajili wa kiungo huyo mwenye kipaji, na medical check-up yake imepangwa hivi karibuni. Wirtz anaweza kuwa nyota mpya katika kiungo cha Liverpool.
Kuondoka kwa Caoimhin Kelleher (Brentford) – Golikipa huyo amekuwa mchezaji wa tatu wa Liverpool kuhamia Brentford kwa mwaka mmoja, akifuatia Sepp van den Berg na Fabio Carvalho.
Usajili wa Mwaka Jana na Matokeo
Giorgi Mamardashvili (Valencia) – Alisajiliwa lakini akakodishwa tena Valencia.
Federico Chiesa (Juventus) – Alikuja kwa matumaini makubwa, lakini hakupata nafasi nyingi kwenye mechi.
Liverpool inaendelea kufanya kazi kwa bidii ili kukamilisha usajili wa wachezaji wengine wanaotarajiwa, ikiwa ni pamoja na beki na kiungo wa ziada, kabla ya msimu mpya kuanza.Ã…

Post a Comment