Ilikuwa asubuhi ya Ijumaa kama kawaida kwenye kisiwa cha Kinmen cha Taiwan, kilichoko kilomita chache tu pwani ya China, wakati sauti ya kengele ya maonyo ya shambulio hewa ilivunja utulivu.
Katika ofisi moja ya serikali ya eneo hilo, watu walizima taa zao na kukimbilia chini ya meza. Wengine walikimbilia kwenye maegesho ya chini ya ardhi. Katika hospitali ya karibu, wafanyikazi walikimbilia kutibu wagonjwa waliokuwa wakipenya kwenye milango wakiwa na majeraha yenye damu.
Lakini damu hiyo ilikuwa bandia, na majeraha hayo yalikuwa ya watu waliojiunga kwa hiari kuigiza. Pamoja na wafanyikazi wa serikali, walikuwa wanashiriki katika mazoezi ya lazima ya ulinzi wa raia na ya kijeshi yaliyofanyika Taiwan mwezi uliopita.
Lengo lake? Kuigiza na kujitayarisha kwa majibu ya kuwazi kwa shambulio la China.

Post a Comment