Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi, na Rais wa China, Xi Jinping, wanatarajiwa kukutana kandokando ya Mkutano wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Shanghai (SCO) utakaofanyika Tianjin, China, tarehe 31 Agosti. Taarifa hiyo imethibitishwa mapema leo na Katibu wa Masuala ya Nje wa India, Vikram Misri.
Hatua hii inajiri wakati India na China zikijitahidi kurekebisha uhusiano wao wa pande mbili huku Rais wa Marekani, Donald Trump, akiendeleza vita vya ushuru ambavyo vimezua mvutano wa kijiografia duniani.
Waziri Mkuu Modi atakuwa nchini China kuanzia Agosti 31 hadi Septemba 1 kwa ajili ya Mkutano wa SCO, ambao utawahusisha viongozi takribani 20 wa dunia, wakiwemo Rais wa Urusi, Vladimir Putin.
Ni jambo la muhimu kutambua kuwa, Waziri Mkuu Modi na Rais Xi watakutana kwa mara ya kwanza baada ya mwaka mmoja, katika ziara ambayo pia itakuwa ya kwanza kwa Modi kutembelea China baada ya kipindi cha miaka saba.

Post a Comment