Awali, Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Shirika la Reli nchini (TRC), Fredy Mwanjala aliiambia TBC kuwa kusitishwa kwa safari hizo kumesababishwa na changamoto za kiufundi ambazo mafundi wa shirika hilo wanashughulikia.
Muda mfupi baadae, Wizara ya Uchukuzi imetoa taarifa ya kuwepo kwa hitilafu katika miundombinu ya reli ikiwemo umeme wa TANESCO zilizosababishwa na uwepo wa mvua kubwa zinazoendelea kunyesha zikiambatana na upepo mkali.
Aidha, taarifa hiyo imeeleza kuwa, mvua hizo zimesababisha athari kubwa zaidi zilizokumba maeneo mengine ikiwemo katika madaraja ya reli ya zamani (MGR), Kidete Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro na Gulwe Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma.

Post a Comment