Chini ya makubaliano yaliyopatanishwa na kiongozi wa Belarus Alexander Lukahsenko kutatua mgogoro huo mwishoni mwa Jumamosi, Kremlin ilisema kesi ya jinai dhidi ya Prigozhin itafutwa na wapiganaji wake hawatachukuliwa hatua za kisheria.
Lakini tovuti ya Kommersant, ikinukuu chanzo kisichojulikana, ilisema uamuzi wa kuanzisha kesi ya jinai bado haujafutwa, na uchunguzi wa uasi huo unaendelea. Kiliendelea kunukuu chanzo hicho kikisema muda hautoshi wa kufunga kesi hiyo.
Ili kuwa wazi, maelezo haya yanatoka kwa vyombo vya habari vya Urusi, na bado hatujaweza kuyathibitisha kwa njia huru.
Bado haijulikani ni nini hasa maana ya mpango huo, na bado hatujasikia kutoka kwa Prigozhin au kiongozi wa Urusi Vladimir Putin.
Kiongozi wa Wagner bado hajaonekana popote.
Kremlin alisema wikendi hii kwamba alikuwa akienda Belarusi.
Prigozhin - ambaye hutoa jumbe za sauti kama kawaida yake- hadi sasa hajasema chochote.
Putin kusamehe 'usaliti'?
Ujumbe unakinzana wa Vladimir Putin umekuwa ukizua hisia na kubadilisha mitazamo ya rais wa Urusi.
Hata hivyo, usitarajie kwamba Rais Putin atakubali kwamba mambo yalikuwa mabaya. Kukubali makosa sio mtindo wake.
Je, ni hatua gani itakayofuata ya rais wa Urusi? Kidokezo, pengine, kilikuja katika toleo la hivi punde zaidi la kipindi cha habari cha televisheni Urusi Jumapili usiku.
Akiripoti juu ya ghasia za Wagner, mtangazaji alicheza dondoo kutoka kwa mahojiano ya zamani ya Putin.
"Je, unaweza kusamehe?"
"Ndiyo. Lakini si kila kitu," Putin anajibu.
"Ni nini huwezi kusamehe?"
"Usaliti."
Iwapo Yevgeny Prigozhin alitazama mahojiano hayo hapo nyuma kabla ya uasi wake basi anajua jibu ya kile kinachoweza kumkumba katika siku zijazo endapo mkataba wake na Putin kumaliza uasi hautatekelzwa na Kremlin.


Post a Comment