Rais wa Urusi Vladimir Putin, amesema kuwa kundi la mamluki la Wagner "linafadhiliwa kikamilifu" na serikali ya Urusi.
"Ningependa kila mtu afahamu kwamba kundi zima la Wagner lilifadhiliwa na serikali - na wizara ya ulinzi na bajeti ya serikali.
Tunafadhili kikamilifu kundi hili," alisema wakati wa mkutano wake kwa vikosi vya usalama kupitia televisheni.
"Kuanzia Mei 2022 hadi Mei 2023, serikali ililipa kampuni ya Wagner rubles 86.262bn swa na dola bilioni moja za Kimarekani katika malipo na ziada."
Putin aliongeza mamlaka itachunguza jinsi pesa zilizolipwa kwa Wagner na kiongozi wake zilivyotumika, shirika la habari la Reuters linaripoti.
Huku hayo yakijiri Rais wa Belarus Alexander Lukashenko amesema anataka kufuatilia uzoefu wa kundi la Wagner katika vita na kujifunza kutoka kwao.
Makamanda na wapiganaji wa Wagner wataruhusiwa kwenda uhamishoni Belarus pamoja na kiongozi wao, Yevgeny Prigozhin, chini ya makubaliano na Moscow yaliyosimamiwa na Lukasjenko
"Kama makamanda wao watakuja kwetu na kutusaidia... tuambie ni nini muhimu kwa sasa... hiyo ni ya thamani. Hilo ndilo tunalohitaji kuchukua kutoka kwa Wagner," Lukasjenko alisema wakati wa mkutano na waziri wake wa ulinzi, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya serikali.
Ameongeza kuwa hana sababu yoyote ya kuogopa uwepo wao na kwamba mamlaka ya Belarus "itawafuatilia kwa karibu".

Post a Comment