Klabu ya Paris St-Germain ya nchini Ufaransa huenda ikaamua kumuuza mchezaje wake Kylian Mbappe msimu huu wa joto badala ya hatari ya kumpoteza bila malipo katika muda wa mwaka mmoja, hatua hii ikija baada ya mchezaji huyo kuiambia klabu hiyo kuwa hataongeza mkataba wake.
Mkataba wake wa sasa unamalizika mwishoni mwa msimu ujao akiwa na chaguo la kuongeza mwaka mwingine katika klabu hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa, kulikuwepo na makataa ya Julai 31 kwa Mbappe, 24, kuiambia PSG iwapo alikuwa anawazia kufanya mkataba wake upya hadi mwaka wa 2025.
Baada ya mazungumzo ya miezi kadhaa, mchezaji huyo ameitumia klabu hiyo barua akisema hatofanya hivyo.
Mfungaji huyo bora wa PSG atakuwa huru kuondoka bila malipo mwishoni mwa msimu ujao na hatua hiyo inaweza kuwa mbinu ya kufanya mazungumzo.

Post a Comment