Chelsea na klabu ya Saudia Al-Hilal zimeanza mchakato wa kujaribu kumsajili mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 24, ambaye hajasafiri na Paris St-Germain katika ziara yao ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi huko barani Asia. (RMC Sport)
Al-Hilal wamempa Mbappe ofa ile ile waliyotoa kwa Lionel Messi - euro 400m (£346.3m) kwa mwaka hadi 2026, ingawa kimsingi ana makubaliano ya kujiunga na Real Madrid kama mchezaji huru msimu ujao wa joto. (Nicolo Schira)
Mbappe yuko tayari kukaa nje kwa msimu mzima na kuondoka PSG bure msimu ujao baada ya mabingwa hao wa Ufaransa kumuweka sokoni Ijumaa. (Sky Sports)

Post a Comment