Jumuiya ya Afrika Mashariki kupitia tume ya Bonde la Ziwa Victoria (LVBC), imesema hatua hiyo ni muhimu na inaweza kusaidia kuokoa maisha ya watu. Wiki mbili tu zilizopita waumini 14 wengi wao wakiwa ni watoto walikufa maji wilayani Bunda, mkoani Mara, Tanzania baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kupinduka kutokana na upepo mkali. Siku moja baadaye wavuvi wengine 20 walikufa maji upande wa Uganda.
Ajali zote mbili zilitokana na upakiaji kupita kiasi na hali mbaya ya hewa. Ziwa Victoria ambalo ni ziwa kubwa zaidi barani Afrika, limeshuhudia maafa mengi ya aina hiyo yanayosababisha vifo vya mamia ya watu. Inakadiriwa kuwa karibu watu 5,000 hupoteza maisha kila mwaka katika ziwa hilo.
.jpeg)
Post a Comment