Manchester City wanaanza kutetea taji lao la Ligi ya Mabingwa wiki hii wakati mechi za makundi zikianza. Kikosi cha Pep Guardiola kimeungana na Arsenal, Manchester United na Newcastle kutoka Ligi Kuu ya Uingereza, huku Newcastle wakirejea katika ligi hiyo baada ya kukosekana kwa miaka 20.
Hizi hapa ni taarifa zote muhimu kuhusu Ligi ya Mabingwa 2023-24. Timu gani ipo katika kundi lipi?
Newcastle wamepangwa Kundi F pamoja na mabingwa wa Ufaransa Paris St-Germain, miamba wa Italia AC Milan na washindi wa zamani wa Ligi ya Mabingwa, Borussia Dortmund.
City watakuwa Kundi G, likionekana kuwa sio kundi gumu - watakapomenyana na RB Leipzig, Red Star Belgrade na Young Boys.
Post a Comment