Katika ligi hii hakuna matarajio ya kumwona Cristiano Ronaldo wala Lionel Messi, hakuna hata mmoja atakayeshiriki Ligi ya Mabingwa msimu huu.
Ronaldo alikuwa mmoja wa watu wa kwanza wenye majina makubwa kuhamia Saudi Arabia – anachezea Al Nassr – wakati Messi yuko Marekani na Inter Miami.
Wengine watakao kosekana ni mchezaji wa Brazil, Neymar na mshambuliaji wa Ufaransa, Karim Benzema wamejiunga na Ronaldo kwenye Ligi ya Saudia. Wako pamoja na Al Hilal na Al-Ittihad.
Lakini bado tutaona baadhi ya majina makubwa ya wakati huu, mshambuliaji wa Ufaransa, Kylian Mbappe akiwa PSG na mpachika mabao wa Man City, Erling Haaland akitafuta kuvunja rekodi zaidi.
Lamine Yamal mchezaji mwenye umri wa miaka 16 mwaka huu alikua mchezaji mdogo zaidi wa Barcelona kwa wakati wote na pia ni mchezaji mdogo zaidi na mfungaji mdogo zaidi wa Uhispania.
.jpeg)
Post a Comment