Atletico Madrid wamemsajili kiungo wa kati wa Uingereza Conor Gallagher kutoka Chelsea kwa mkataba wa miaka mitano, LaLiga na vilabu vya Premier League vilisema Jumatano.
Gallagher, ambaye alikuwa Chelsea tangu umri wa miaka minane, amesaini mkataba hadi 2029 na Atletico ambao wamelipa euro milioni 42 kwa mchezaji huyo wa miaka 24, kulingana na ripoti za vyombo vya habari.
"Tunamtakia Conor kila la kheri anapoanza ukurasa mpya katika maisha yake ya soka," Chelsea ilisema katika tangazo rasmi lililochapishwa kwenye tovuti yao.

Post a Comment