Rais wa Marekani Donald Trump anasema "kitu kizuri huenda kinatokea" kufuatia mazungumzo jana jijini Geneva kuhusu mpango wa kumaliza vita vya Urusi nchini Ukraine. Viongozi wa Umoja wa Ulaya wanakutana kwa mazungumzo zaidi leo baada ya wajumbe wa Marekani na Ukraine kurudi nyumbani.
Serikali ya Urusu inasema pendekezo la Marekani la kumaliza vita vya Ukraine "kimsingi, linaweza kuwa msingi wa makubaliano ya mwisho ya amani." Rais Vladimir Putin wa Urusi alisema toleo la mpango huo ulioonekana na Urusi "linafanana na mazungumzo" yaliyofanyika kwenye mkutano wa Marekani-Urusi huko Alaska mapema mwaka huu.

Post a Comment