#-----------Start surfernetwork.com--------------- # Ads.txt last updated on:  2026/06/10 13:26:00.23423 by surfernetwork.com MANAGERDOMAIN=surfernetwork.com CONTACT=support@surfernetwork.com # SurferNETWORK surfernetwork.com, 204, DIRECT # Adswizz adswizz.com, 724, RESELLER, 52ded3ee71b94c84 #Azerion targetspot.com, 455, RESELLER, feb28ed826dcf532 improvedigital.com, 2734, RESELLER adswizz.com, 172, RESELLER, 52ded3ee71b94c84 appnexus.com, 7265, RESELLER, f5ab79cb980f11d1 tritondigital.com, 44733, RESELLER, 19b4454d0b87b58b rubiconproject.com, 9753, RESELLER, 0bfd66d529a55807 #US rubiconproject.com, 16418, RESELLER, 0bfd66d529a55807 #EMEA # DAX thisisdax.com, 5460, RESELLER thisisdax.com, 5461, RESELLER # katz Katzdigital.com, 318, RESELLER Katzdigital.com, 80, RESELLER # Magnite rubiconproject.com, 8441, RESELLER, 0bfd66d529a55807 #-----------End surfernetwork.com-----------------

JIJI LA ARUSHA NA APICARE INTERNATIONAL KUANZISHA MRADI WA UTALII WA NYUKI KUCHOCHEA UCHUMI NA AJIRA

 



Jiji la Arusha kwa kushirikiana na taasisi ya kimataifa ya Apicare International limeanza maandalizi ya kuanzisha mradi wa utalii wa nyuki katika maeneo ya Bonde la Mto Naura, Mto Themi pamoja na Mlima Suye, ikiwa ni mkakati mahsusi wa kuongeza vivutio vya utalii na kuimarisha uchumi wa wananchi.
Mradi huo wa kipekee unatarajiwa kuwa chachu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wakazi wa Arusha kwa kuunganisha uhifadhi wa mazingira, ufugaji wa nyuki na shughuli za utalii. Kupitia mradi huo, wageni wa ndani na nje ya nchi watapata fursa ya kujifunza kuhusu uzalishaji wa asali, umuhimu wa nyuki katika uhifadhi wa mazingira, pamoja na kushiriki uzoefu wa kiutalii unaohusisha mazingira asilia ya Jiji la Arusha.
Aidha, mradi huo unalenga:
• Kutoa ajira kwa vijana na wanawake
• Kuongeza kipato cha wafugaji wa nyuki
• Kuhamasisha uhifadhi wa mito na misitu
• Kuongeza mapato ya Jiji kupitia utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
Bonde la Mto Naura na Mto Themi pamoja na Mlima Suye ni maeneo yenye mandhari ya kuvutia na umuhimu mkubwa wa kiikolojia, hivyo kuifanya Arusha kuendelea kujiimarisha kama kitovu cha utalii si tu wa wanyamapori bali pia utalii wa kiikolojia na kilimo.
Hatua hii inaonyesha dhamira ya Jiji la Arusha katika kubuni miradi bunifu ya maendeleo inayolenga kuinua uchumi wa wananchi sambamba na kulinda mazingira kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Mobile Logo Settings

Usa River Tv