Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Nicholous Merinyo Mkapa, aliyemwakilisha Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb.) katika sherehe za Maadhimisho ya siku ya Usalama Mtandaoni (Safer Internet Day) tarehe 10 Februari 2027, Ukumbi wa Auditorium - UDOM, Dodoma.
Maadhimisho hayo yaliyoongozwa na kaulimbiu isemayo “Teknolojia Mahiri, Machaguo Salama: Tuwalinde Watoto katika Zama za Akili Unde,” ililenga kuhamasisha jamii kuchukua tahadhari dhidi ya hatari zinazoweza kujitokeza kutokana na matumizi yasiyo salama ya teknolojia za kisasa, hususan Akili Unde (AI).

Post a Comment