Kwa mara nyingine tena, wakati wa Pasaka unapokaribia, mioyo ya waumini inaelekezwa kwenye rehema za Mungu kupitia tamasha la kiroho linalongojelewa kwa hamu kubwa. Usiku Kimataifa wa Rehema (INOM) 2026 unatarajiwa kufanyika tena mwaka huu, ukiwa na lengo la kuleta wokovu, uponyaji na ukombozi kwa wengi.
Tukio hili kubwa la kiroho linaloandaliwa na Kanisa la Christ Mandate kupitia kiongozi wake, Dr. Malachi Joseph, litafanyika Ijumaa Kuu (Good Friday) katika eneo la Bunju B, Katavi Street – Christ Mandate City.
Nyota wa Muziki wa Injili Kukaribishwa
Usiku huu wa pekee utakuwa na burudani ya kiroho itakayotolewa na waimbaji mashuhuri wa injili nchini ambao ni:
Rose Mhando – anayejulikana kwa sauti yake ya kupenya na nyimbo zenye nguvu za kiroho
John Lissu – msanii mwenye uzoefu anayeleta ujumbe wa imani kupitia nyimbo zake
Vinance Malachi – mwanamuziki anayeendelea kujipatia umaarufu kwa nyimbo zake zenye kina cha kiroho
Agape Gospel Band – bendi inayojulikana kwa uchezaji bora na kusindikiza nyimbo za injili kwa ubora wa hali ya juu
Na wengine wengi watakaotangazwa
Maana ya Usiku wa Rehema
Usiku wa Rehema (International Night of Mercy – INOM) ni mkutano maalum wa maombi na sifa unaolenga kuwakutanisha waumini katika hali ya toba na kusihi rehema za Mungu. Katika muktadha wa Kikristo, hasa wakati wa kukumbuka mateso na kifo cha Yesu Kristo, wakati huu ni wa kutafakari upendo na rehema alizoonyesha kwa wanadamu.
Maandalizi na Mwaliko
Waandalizi wanatoa wito kwa wote kujitayarisha kiroho na kimwili kwa ajili ya usiku huu wa baraka.
"Usikose katika Usiku huu wa Rehema; USIKU WA REHEMA! JIANDAE!" – ndio kaulimbiu inayowavutia wengi kuhudhuria.

Post a Comment