Shirika la Care Home for Children Organization limepata heshima ya kushiriki katika tukio muhimu la kijamii lililoandaliwa na Sam One Africa. Tukio hilo lilihusisha ugawaji wa taulo za kike, upandaji miti, pamoja na utoaji wa elimu ya afya. Ilikuwa siku yenye matokeo chanya na ya baraka kubwa.
Kupitia tukio hili, tuliweza kugusa maisha ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kiloleli kwa kuwapatia elimu na msaada muhimu.
Tunatoa shukrani za dhati kwa nafasi hii na kwa wote waliochangia kufanikisha tukio hili muhimu.

Post a Comment