Katika kumbukizi hii ya kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo, taasisi inapenda kutumia fursa hii kuwakumbusha wafanyakazi wake, wahudumu wa kujitolea (volunteers), pamoja na jumuiya nzima ya familia hii, kwamba ufufuko huu unapaswa kwenda mbali zaidi ya kuviringishwa kwa jiwe zito lililowekwa mbele ya kaburi la Mwana wa Mungu.
Nguvu iliyoweza kuvingirisha jiwe lile inapaswa kuingia ndani yetu, ikaviringisha mioyo yetu iliyo migumu, na kutufanya kuwa viumbe wapya—waliojaa upendo, kujali, na kutenda sawasawa na mapenzi ya Yeye aliyetuumba.
Kama tulivyoendelea kusisitiza mara kwa mara, CARE HOME FOR THE CHILDREN ni taasisi isiyofungamana na dini wala upande wowote linapokuja suala la kusaidia watoto wenye uhitaji na kuleta mabadiliko chanya ndani ya jamii tunayoishi. Huo ndio msimamo wetu—leo, kesho, na hata milele.
Ndugu wanafamilia, kwa maneno haya machache, taasisi inapenda kuwatakia sherehe njema za Sikukuu hii. Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema, aendelee kuwalinda na kuwabariki siku hii muhimu na katika maisha yenu yote.
Imeandaliwa na:
Edward Julius Ager (Mzalendo)
~ Volunteer ~

Post a Comment