#-----------Start surfernetwork.com--------------- # Ads.txt last updated on:  2026/06/10 13:26:00.23423 by surfernetwork.com MANAGERDOMAIN=surfernetwork.com CONTACT=support@surfernetwork.com # SurferNETWORK surfernetwork.com, 204, DIRECT # Adswizz adswizz.com, 724, RESELLER, 52ded3ee71b94c84 #Azerion targetspot.com, 455, RESELLER, feb28ed826dcf532 improvedigital.com, 2734, RESELLER adswizz.com, 172, RESELLER, 52ded3ee71b94c84 appnexus.com, 7265, RESELLER, f5ab79cb980f11d1 tritondigital.com, 44733, RESELLER, 19b4454d0b87b58b rubiconproject.com, 9753, RESELLER, 0bfd66d529a55807 #US rubiconproject.com, 16418, RESELLER, 0bfd66d529a55807 #EMEA # DAX thisisdax.com, 5460, RESELLER thisisdax.com, 5461, RESELLER # katz Katzdigital.com, 318, RESELLER Katzdigital.com, 80, RESELLER # Magnite rubiconproject.com, 8441, RESELLER, 0bfd66d529a55807 #-----------End surfernetwork.com-----------------

Adaiwa kumuua mpangaji mwenzake kisa Sh1,000 ya umeme


Jeshi la Polisi Mkoa Arusha, linamshikia msichana Brandina Fred mkazi wa Kijiji cha IIkirev, Kata ya Olturoto wilayani Arumeru, kwa tuhuma za kumuuwa kwa kumchoma kisu mpangaji mwenzake, Erick Adam kutokana mchango wa sh 1000 za umeme.


Tukio hilo limetokea jana baada ya kutokea ugomvi baina ya wapangaji hao wawili ambapo inadaiwa marehemu Adam aligoma kulipia deni la umeme ambao kwa kawaida wapangaji huchangia.


Kamanda wa polisi mkoa Arusha, Justine Masejo akizungumza na Mwananchi leo, June 20, 2023, amesema tukio hilo lilitokea majina ya mchana wakati, Blandina akiwa na kisu akijiandaa na kupika.


"Kilichotokea ni kuwa wote ni wapangaji walikuwa wakigombana huyu binti alikuwa na kisu kwa kuwa alikuwa jikoni, sasa ndio alimchoma mwenzake," amesema

Amesema Adam alifariki kutokana na kutokwa na damu nyingi baada ya kuchomwa kisu.

Kamanda Masejo amesema, Jeshi hilo bado linamshikilia kwa mahojiano, mtuhumiwa huyo na bado anahojiwa kuhusiana na tuhuma hizo.

"Taratibu zikikamilika atafikishwa mahakamani kutokana na tuhuma ambazo zinamkabili," amesema kamanda huyo, na kwamba mwili wa Adam umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mountmeru kwa uchunguzi zaidi.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Mobile Logo Settings

Usa River Tv