Katika kikao hicho, amewakaribisha watumishi hao na kuwapongeza kwa kuaminiwa kujiunga na utumishi wa umma, huku akiwataka kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na kuwajibika kwa maslahi ya wananchi.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuzingatia maadili ya kazi, kufuata sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma pamoja na kushirikiana na jamii ili kuleta maendeleo katika sekta ya elimu wilayani humo.
Pia amewataka kutumia taaluma zao kuboresha kiwango cha elimu na kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya kujifunzia.
Post a Comment